May 27, 2012
ANASWA AKITUHUMIWA KUVUNJA NEEMA CRAFTS IRINGA
| UNAMAONI GANI ? |
BREAKINGNEWS.....RAIA WA INDIA ADAIWA KUNYANYASA WANAWAKE IRINGA ANAMILIKI MAHABUSU BINAFSI ,POLISI WAMSAKA
JESHI la polisi mkoani Iringa linamsaka mkurugenzi wa taasisi ya mikopo ya Brac ambaye ni Raia wa India kwa tuhuma za kumnyanyasa kwa kumfungia katika mahabusu binafsi ofisini kwake mwanamke mmoja Edina Panzi (47) mkazi wa Ilala katika Manispaa ya Iringa akimdai kiasi cha shilingi 5800 .
Kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Peter Kakamba alisema kuwa raia huyo wa India anasakwa na jeshi la polisi mkoani Iringa baada ya kumfungia katika mahabusu mwanamke huyo ambaye alikopeshwa fedha na taasisi yake hiyo ya Brac tawi la Ilala mjini Iringa.
Bila kumtaja jina raia huyo wa India ,kamanda Kakamba alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 11 jioni katika eneo la Ilala ambako zipo ofisi za taasisi hiyo ya Brac baada ya jeshi la polisi kupata taarifa kutoka kwa rai wema kuhusiana na mwanamke huyo kufungia katika mahabusu katika ofisi hiyo kabla ya polisi kufika kumfungulia mlango mwanamke huyo.
"Jeshi la polisi lilipata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuhusuana na mwanamke huyo kufungia katika mahabusu hiyo kwa sababu ambavyo raia huyo wa India anazijua yeye na ndipo polisi walipofika na kufanikiwa kufungua mahabusu hiyo na kumtoa mwamamke huyo "
Kakamba alisema kuwa taasisi hiyo imekuwa ikijishughulisha na utoaji wa mikopo kwa wanawake jambo ambalo si baya ila ubaya unakuja pale ambapo mkopeshaji huyo anajichukulia sheria mkononi kwa kutoa adhabu iliyo kinyume na sheria za nchi hii kwa kuwafungia mahabusu wakopaji wake.
Kwani alisema kuwa haipo sheria inayomruhusu mtu awaye yeyote yule ama taasisi ya ulinzi kumiliki mahabusu kwa kukamata watu na kuwafungia mahabusu kwani kufanya hivyo ni kosa na wanapatikana na tuhuma kama hizo wakikamatwa hufikishwa mahakamani.
Hivyo alisema kuwa jeshi la polisi linaendesha msako mkali wa kumsaka mkurugenzi huyo wa Brac ambaye ni rai wa India ili kufikishwa mahakamani .
Kwa upande wake mwanamke huyo anayedaiwa kufungiwa mahabusu alisema kuwa alifungiwa katika mahabusu hiyo juzi kuanzia majira ya saa 4 asubuhi hadi saa 11 jioni kabla ya waandishi wa habari wa mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) kuweza kufika eneo hilo na kutoa taarifa hiyo polisi .
Mwanamke huyo alisema kuwa jumla ya deni lote alilokopa lilikuwa ni kiasi cha shilingi 500,000 na hadi anakamatwa na kufungiwa katika mahabusu hiyo alikuwa akidaiwa kiasi cha shilingi 5800 pekee .
Diwani wa kata hiyo ya Ilala ambaye pia ni naibu meya wa Manispaa ya Iringa Grevas Ndaki alisema kuwa uongozi wa kata hiyo hauungi mkono hata kidogo unyanyasaji unaofanywa na Raia huyo wa India kwa wanawake wa kata hiyo na kuwa kutokana na tabia hiyo kuendelea kuchukua kasi wanaona ni vema ofisi hiyo kuondolewa katika kata hiyo .
| UNAMAONI GANI ? |
TAARIFA KUTOKA TFF LEO

| UNAMAONI GANI ? |
KAMPUNI YA SIMU YA AIRTEL YAMUUNGANO MKONO MBUNGE PROF MSOLLA JIMBONI
MBUNGE wa jimbo la Kilolo mkoani Iringa Profesa Peter Msolla amekabidhi msaada wa kompyuta tatu na vitabu vya kiada msaada wenye thamani ya shilingi milioni 9 uliotolewa na kampuni ya simu ya airtel katika shule tatu za sekondari jimboni kwake .
Akikabidhi msaada huo katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya shule ya Sekondari Mazombe juzi ,Prof.Msolla alisema kuwa msaada huo ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi zake katika kuendeleza elimu kwa wananchi wake.
Prof Msolla alisema kuwa mbali ya kuwa shule hiyo ya sekondari Mazombe haina umeme ila ametanguliza kompyuta hizo kama njia ya kuanza mkakati wa kuisaidia shule hiyo kupata umeme wa mionzi ya juu ,umeme ambao atasaidia kuufunga katika shule hiyo.
Alisema kuwa shule hiyo ilikuwa ikikabiliwa na tatizo la kompyuta na kupelekea walimu kushindwa kuchapa mitihani ama kuandaa masomo yao kwa kutumia kompyuta na kuishia kuandaa mitihani na vipindi mbali mbali kwa kuandika kwa mkono jambo ambalo lilikuwa likikwamisha shughuli mbali mbali shuleni hapo.
Mbunge Prof Msolla alisema msaada huo wa kompyuta na vitabu vya kiada katika shule hiyo na shule ya Sekondari Maria Consolata , Udzungwa na Mazombe umetolewa na kampuni ya simu ya airtel Tanzania .
"Napenda kulipongeza sana kampuni ya simu ya airtel kwa kusaidia maendeleo ya elimu katika jimbo langu .....ndugu zangu wanafunzi na wazazi moja kati ya vipaumbele vyangu vilikuwa ni elimu na wakati nikiingia madarakani mwaka 2005 Kilolo ilikuwa na shule za sekondari tatu ila sasa tumepiga hatua na kuwa na shule zaidi ya 20 ....napenda kuwahakikishieni kuwa tutaendelea kupiga hatua katika maendeleo ya elimu "
Pia aliwataka wanafunzi kutumia vizuri nafasi hiyo waliyoipata kwa kuendelea kusoma kwa juhudi kubwa na kuwa katika dunia ya sasa elimu ndio kila kitu na bila elimu ni vigumu kuweza kufanikiwa .
Awali mwakilishi wa artel mkoa wa Iringa Bi Hildegrad Ntamuturano alisema kuwa kampuni yake imeendelea kusaidia jamii katika mambo mbali mbali na kuwa mbali ya msaada huo wa vitabu na kompyuta bado wataendelea kusaidia katika maeneo mengine ya kijamii hapa nchini .
Akishukuru kwa msaada huo kwa niaba ya walimu wakuu wenzake mkuu wa shule ya sekondari Maria Consolata Bw. Mufwalamagoha Kibasa alisema kuwa jitihada zinazofanywa na mbunge Prof Msolla katika jimbo hilo ni mfano wa kuigwa kwa wabunge wengine na kuwa kati ya vitu vizuri ambavyo wabunge wanapaswa kutambua ni elimu hivyo ni vema kuelekeza nguvu zao katika kusaidia elimu.
| UNAMAONI GANI ? |
ZITTO KABWE ASEMA MAFUTA KUWA SUALA LA MUUNGANO NI KOSA
- Kila upande wa Muungano uchimbe Mafuta na Gesi Asili yake na Mapato yawe ya Serikali ya upande husika.
- Shughuli za Utafutaji kwenye vitalu vyenye mgogoro ziendelee mara moja
- Zanzibar ianzishe Shirika lake la Mafuta (PetroZan)
- Katiba mpya itofautishe utafutaji (upstream) na Biashara (uchimbaji, midstream na downstream)
| UNAMAONI GANI ? |
May 26, 2012
MISS DAR INTER COLLEGE KURINDIMA JUNI 8 CLUB SUNCIRO
SHINDANO la kumsaka Miss Dar Intercollege 2012 linatarajiwa kufanyika Juni 8 kwenye ukumbi wa Sunciro, ulipo Sinza Shekilango jijini Dar es Salaam, imefahamika.
Mratibu wa Shindano hilo Dina Ismail alisema jana kwamba warembo watakaoshiriki shindano hilo wanaendeleza na mazoezi kwenye hoteli ya Lamada jijini Dar es Salaam chini ya ukufunzi wa Marylidya Boniface, huku kwa upande wa shoo wakinolewa na Bob Rich.
Alisema mpaka sasa warembo 12 kutoka vyuo vya Biashara (CBE), Uandishi wa Habari (DSJ) na Time, Ustawi wa Jamii na kile cha Usimamizi wa Fedha (IFM) wamesharipoti kambini.
Dina aliwataja warembo hao kuwa ni pamoja na Hilda Edward, Nancy Maganga, Saada Seleman, Neema Nashon, Rose Muchunguzi, Fina Revocatus,Jane Augustino,Theresia Issaya na Natasha Deo.Taji la kitongoji hicho linashikiliwa na Rose Msuya kutoka IFM.
Kwa upande mwingine, mratibu huyo ameyaomba makampuni mbalimbali kujitokeza kudhamini shindano hilo ambalo linatarajiwa kuwa la aina yake na hasa ikizingatiwa kuwa washiriki wake wana vigezo vya hali ya juu.
“Tunaomba makampuni mbalimbali yajitokeze kudhamini shindano letu…mpaka sasa wadhamini tulionao ni pamoja na kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Redd’s, Lamada Hotel, Ndege Insurance, Dodoma Wine na Clouds Fm| UNAMAONI GANI ? |
HAPPY BATHIDAY YA AMINA SHAMTE YATIKISA IRINGA
| UNAMAONI GANI ? |
TULLO CHAMBO AULA TASWA
CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) kinatoa pongezi kwa Mhariri wa Habari za Michezo wa gazeti la Tanzania Daima, Tullo Chambo kwa kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Riadha Tanzania (RT).
Chambo alitwaa nafasi hiyo kwenye Uchaguzi Mkuu wa RT uliofanyika Jumapili mjini Morogoro, ambapo ni miongoni mwa wajumbe wapya walioingia kwenye chama hicho.
Wengine walioshinda ni Anthony Mtaka ambaye anakuwa Rais mpya wa RT, wakati Makamu wa Rais Utawala ni William Kallaghe, Makamu wa Rais Ufundi, Dk. Ahmed Ndee, Katibu Mkuu, Suleiman Nyambui, Katibu Msaidizi, Ombeni Zavalla, Mhazini, Is-Haq Suleiman.
Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ni Mwinga Mwanjala, Meta Petro, Peter Mwita, Rehema Killo, Lwiza John, Zakaria Barrie, Zakaria Gwanda, Robert Kalyahe na Christian Matembo.
TASWA inatambua Chambo ni mwanahabari mzoefu, ambaye kwa muda mrefu amekuwa mhariri wa habari za michezo na ni mtu mwenye kujua mambo mengi yanayohusu riadha, hivyo atakuwa kiungo muhimu kwa watu wa riadha, pia atakuwa kiongo kizuri kwa waandishi wa habari za michezo kuhusiana na mambo ya riadha.
TASWA inaahidi kumpa ushirikiano wa kutosha kadri itakavyoweza na inamtakia kila la heri, huku ikiamini hatawaangusha Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa RT waliomuamini wakamchagua kushika wadhifa huo.
Pia Taswa inawapongeza viongozi wote wa RT walioingia madarakani Jumapili, ikiamini watakuwa chachu ya mafanikio ya riadha hapa nchini.
Nawasilisha.
Amir Mhando
Katibu Mkuu TASWA
25/05/2012
| UNAMAONI GANI ? |
WANANCHI RUAHA MBUYUNI WADAI WAMEKUWA WAKIUZIWA MAJI YA MTO
Wananchi wa Ruaha mbuyuni jimbo la Kilolo mkoani wamelalamikia hatua ya uongozi wa kijiji hicho kuwauzia maji wanayochota katika mto Ruaha jambo ambalo wamedai kuwa ni sawa na unyanyasaji .
Wakizungumza katika mdahalo ulioandaliwa na azaki za kiraia mkoa wa Iringa mdahalo ulioendeshwa na asasi ya Isico katika ukumbi wa Upendo Ruaha Mbuyuni leo .
Wananchi hao wamesema kuwa wanashangazwa na ufisadi unaofanywa na viongozi wa kijiji hicho kwa kuwauzia ndoo moja ya maji wanayochota katika mto Ruah kiasi cha shilingi 200 jambo ambalo wao wanalifananisha na ufisadi na unyanyasaji mkubwa.
Hivyo walihoji sababu ya uongozi wa kijiji hicho kuwauzia maji ambayo si ya bomba ni maji yanayochota katika mto .
Kutokana na hali hiyo wameiomba asasi hiyo ya Isico kufikisha kilio chao hicho kwa mbunge wao Prof Peter Msolla ambaye alipaswa kushiriki katika mdahalo huo ,ili kuweza kuangalia uwezekano wa kuchimbiwa kisima cha maji safi kutokana na maji wanayotumia sasa kutoka katika mto huo kutokuwa safi na salama.
Mwakilishi wa mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilolo Bw John Kiteve alitaka suala hilo kuweza kuangalia na kuwa si haki kwa kijiji kuwatoza wananchi maji ya mto ambayo .
| UNAMAONI GANI ? |
